TANGAZO

TANGAZO

Matahari...

Aku ingin seperti matahari...

Puisi Untuk Mama Papa

Senja tadi mataku berkaca-kaca dan dadaku sesak karna menahan tangis Meski ku tau ini adalah tangis bahagia dan tanda kesyukuranku karena memiliki kalian

Tips dan Trik Memulai Skripsi sampai sidang Skripsi

Saya memulai menulis ini dengan senyum-senyum sendiri. Serasa ada yang ngomong dalam diri sendiri, “gaya beud sih?” He”.

Presentasi tentang Ulangan Online di SMA 3 Jakarta 28 Sept 2012

Berawal dari ajakan Dosen Pembimbing skripsi saya (Bu Muti) yang mengajak saya untuk sharing tentang pembuatan ulangan online

This Is The Real Never Ending Process: Learning The Qur’an

“Sebaik-baik kaliah adalah orang yang belajar Al-Qur’an dan mengajarkannya” Hr. Al-Bukhari

Kultwit #Nikah oleh Ust. Salim A Fillah

Sekarang emang lagi zamannya nge-twit... Nah, Ustadz yang satu ini paling sering ngetwit...

Friday, 22 August 2014

WOLPER NDIO MSANII ANAEONGOZA KWA KUBADILI .........?>>>>.


KUNA nini kwani? Staa wa sinema za Bongo, Jacqueline Wolper anatajwa kuongoza wasanii wenzake kwa kubadili namba za simu za mkononi huku baadhi ya mashoga zake wakijiuliza kulikoni?

Staa wa sinema za Bongo, Jacqueline Wolper.

Kwa mujibu wa rafiki mmoja wa karibu na Wolper (jina lipo), anamshangaa sana shoga yake huyo kwani amekuwa akibadili namba za simu kwa mwaka mmoja hata mara saba. 


“Unajua kwa maisha ya sasa, simu ikipotea mtu unairinyuu laini yako ileile, maana ndiyo inayojulikana na wadau. Lakini yule mwenzetu siyo. Nimeshamsevu kwenye simu yangu kwa majina ya Wolper, Wolper Tena, Wolper Nyingine, Wolper Nyingine Kabisa na Wolper Hakuna Tena, lakini zote kwa sasa hazipo hewani,” alisema shoga yake huyo huku akicheka.Wolper alipotafutwa kwa simu yake ya mkononi iliyozoeleka, hakupatikana. Jitihadi zilifanyika akaja kupatikana kwenye namba mpya ambapo alisema:
“Mimi nikishapoteza laini naona uvivu kwenda kuirinyuu, ndiyo maana nanunua nyingine.”

SOMA HOTUBA YA MWISHO YA KANALI MUAMAR GHADAFI KABLA HAJATANGULIA MBELE YA HAKI! MY HERO SALUTE!!



Hotuba ya Mwisho ya Kanari Muammar Gafafi enzi za uhai wake,watanzania tunalojambo la kujifunza.
Alianza hivi,
 
"Kwa jina la Mwenyezi Mungu
(Allah), Mungu mpaji, na mwenye
rehema....


Kwa miaka takribani 40 ama ilikuwa
zaidi sikumbuki. Nachokumbuka ni
kuwa nilifanya kila nilichoweza
kuwapa watu wangu nyumba,
hospitali na shule. Na kila walipohisi
njaa niliwapa chakula. Niliifanya
Benghazi kutoka jangwa kuwa ardhi
nzuri ya kilimo.
Nilisimama imara dhidi ya Ronald
Regan (Rais wa zamani wa
Marekani), alipomuua binti yangu
niliyemuasili. Alikua anajaribu kuniua
mimi lakini akamuua yule binti yatima
masikini. Niliwasaidia kaka na dada
zangu waafrika fedha kupitia AU.
Nilifanya kila nililoweza kuwafanya
watu wangu waelewe maana halisi
ya demokrasia; ambapo watu wa
tabaka la chini niliwapa madaraka.
Lakini hawakuridhika. Hata aliyekuwa
na nyumba ya vyumba kumi, nguo
mpya, na fanicha nzuri, hakuridhika.
Alihitaji zaidi.
Kwa jinsi walivyokuwa wabinafsi
walihitaji zaidi. Hivyo wakawaambia
Marekani kuwa wanataka
"demokrasia" na "uhuru". Hawakujua
kuwa "demokrasia" waliyoitaka ilikua
ni mfumo wa unyonyaji ambapo
mbwa mwenye nguvu zaidi huwala
mbwa wadogo.
Walikua hawasikii wala hawaoni.
Walitaka "demokrasia". Wakasahau
kuwa hata Marekani hakukuwa na
huduma za afya za bure, dawa bure,
elimu bure na chakula cha bure.
(Huduma hizi za bure zilipatikana
Libya tu).
Nchini Marekani mtu masikini/fukara
hana cha bure. Labda awe
ombaomba au avuje jasho kuhemea.
Haikujalisha nilifanya kwa kiasi gani
bado hawakuridhika. Lakini wapo
waliojua mimi ni mtoto wa Gamal
Abdel Nasser, mwarabu pekee halisi
na kiongozi wa kiislamu tuliyewahi
kuwa nae tangu enzi za Salah-al-
Deen.
Wakati Nasser anapigania mfereji wa
Suez kwa watu wake nami nilikua
naipigania Libya kwa watu wangu.
Nilikua najaribu kufuata nyayo zake
ili kuwaweka watu wangu huru
kutoka kwenye makucha ya wakoloni
wanaotuibia.
Lakini kwa sasa niko mateka katikati
ya majeshi makubwa ya dunia katika
historia. Mwanangu mpendwa
mwenye asili ya Afrika, Obama
anataka kuniua.
Ili achukue uhuru wetu, achukue haki
yetu ya huduma za bure za afya,
huduma za bure za elimu, na chakula
chetu; na kutuletea mfumo mpya wa
kimarekani wa kuiba uitwao
"Ubepari"
Lakini wote katika dunia ya tatu
tunajua maana yake. Maana yake ni
kuwa "washirika" wanatawala
mataifa, wanatawala dunia, na watu
wanaishia kuteseka.
Kwa hiyo hakuna mbadala kwangu.
Lazima niwe na msimamo. Na kama
Mungu atapenda nitakufa kwa
mapenzi yake.
Mapenzi yake yaliyofanya nchi yetu
kuwa na ardhi yenye rutuba, chakula
bora, na huduma bora za afya.
Mapenzi ya Allah yaliyowezesha
tukawasaidia kaka na dada zetu
waafrika na waarabu waliokuwa na
shida.
Sipendi kufa; lakini kama nitakufa ili
kuiokoa ardhi hii, kuokoa watu
wangu, na wengine ambao ni kama
wanangu; acha nife.!
Acha sauti hii iwe agano langu kwa
dunia kuwa nilisimama kupinga
uvamizi wa NATO. Nilisimama
kishujaa kupinga usaliti wa nchi za
magharibi na nia mbaya za kikoloni.
Na hapa nimesimama na ndugu
zangu waafrika, kaka na dada zangu
waislamu kama ngao yangu ya
matumaini.
Wakati wengine walipokuwa
wanajenga majumba ya kifahari,
mimi niliishi kwenye nyumba ya
kawaida na kwenye mahema. Siwezi
kusahau maisha yangu ya utoto kule
Sirte.
Sikutapanya rasilimali za nchi yangu
kipumbavu. Na kama alivyokua
Salah-al-Deen, kiongozi wetu katika
uislamu, nilichukua kidogo sana kwa
ajili yangu, na sehemu kubwa
niliwapa wananchi.
Watu wa magharibi wameniita
"kichaa", "mwendawazimu" lakini
wanajua ukweli kuwa mimi si kichaa
wala mwendawazimu; ila waache
waendelee kudanganya. Wanajua hii
ardhi ni huru na haipo kwenye
himaya ya kikoloni. Huu ndio
msimamo wangu na dira yangu na
imekuwa wazi kwa watu wangu.
Nitapambana hadi pumzi yangu ya
mwisho ili watu wangu wawe huru.
Mwenyezi Mungu atusaidie tubaki
waaminifu na tuwe huru.

-- Mu'uammar Qaddafi.

Ndege ya shirika la ndege ya malaysia wakati wa uhai wake.


Ofisa mmoja mwanamke mwenye cheo cha juu katika bankkubwa iliyoko mjini Kuala Lumpur , Malaysia pamoja na mumewe wameshtakiwa kwa kuiba mamilioni ya dola za kimarekani kutoka katika account za abiria na wafanyakazi wa ndege iliyopotea ya Malaysia Air Line MH370 ambayo ilipotea katika mazingira ya kutatanisha,katika bahari ya Hindi mapema mwezi March.
Pamoja na kushtakiwa huko, mtu na mkewe hao waliepuka makosa mengine yapatayo 16 kati ya makosa hayo yamo wizi,kukaidi amri ya mahakama na makosa mengineyo.
Ofisa huyo Nur Shila Kanan anatuhumiwa kutumia cheo chake vibaya katika benki ya HSBC nchini Malaysia kwa kupoka pesa.
Mwendesha mashtaka aliiambia mahakama moja mjini Kuala Lumpur,Malaysia kwamba wawili hao walifanikiwa kukwapua dola za kimarekani elfu thelathini kutoka katika account tatu tofauti za abiria waliopotea na account moja ni ya mfanyakazi wa shirika hilo la Malaysia Air Line.